Polisi nchini Ujerumani wanasema kuwa kumekuwa na shambulizi la kuchoma moto ofisi za gazeti ambalo lilichapisha vibonzo kutoka kwa gazeti la vibonzo la Charlie Hebdo.

Mawe na vitu vinavyowaka moto vilirushwa katika dirisha la ofisi za gazeti la Hambuger Morgenpost mapema leo Jumapili.
Vyumba viwili kwenye afisi hizo viliharibiwa lakini moto huo ulizimwa kwa haraka na hakuna mtu aliyejeruwa.
 
Wiki iliyopita gazeti hilo lilichapisha picha za vibonzo vya mtume Mohammed kutoka gazeti la ufaransa la Charlie Hebdo.
Makala kwenye tovuti ya gazeti hilo inasema haijabainika iwapo shambulizi hilo lina uhusiano na kuchapishwa kwa picha hizo.
Polisi mjni Hamburg wanasema kuwa wamewakamata vijana kufuatia kisa hicho.




Credit; BBC
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment