FEDERER NA DJOKOVIC WAENDELEZA USHINDI


Roger Federer kushoto na Novak Djokovic wakisalimiana katika moja ya mashindano.
Nyota wa tenisi Roger Federer ameendeleza ushindi kwa asilimia mia katika mashindano ya wanaume ya tenisi ya dunia.
Federer alianza kwa kushinda seti ya kwanza kwa 7-5 kisha akapoteza seti ya pili kwa 4-6 kisha akamaliza kwa ushindi wa seti 6-4, dhidi ya Kei Nishikori wa Japan.


Roger Federer
Naye Novak Djokovic ambaye ni nyota namba moja kwa ubora aliendeleza wimbi la ushindi katika michuano hiyo kwa kumchapa Tomas Berdych.
Djockovic alipata ushindi wa seti mbili ambapo seti ya kwanza alishinda kwa 6-3 na kisha akamaliza kwa 7-5.
Novak Djokovic
Djokovic atachuana na Rafael Nadal siku ya jumamosi huku Roger Federer akimsubiri mshindi wa Ijumaa kati ya Andy Murray au Stan Wawrinka.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment