HILI NDILO JENGO REFU KULIKO YOTE DUNIANI

Burj Khalifa jengo ambalo ni refu kuliko majengo yote duniani ambalo linapatikana jijini Dubai.


Kwa hesabu za haraka haraka, urefu wa mita 829.8 (sawa na futi 2,722) ni sawa sawa na viwanja vinane vya mpira wa miguu..
Uwanja wa mpira wa miguu uliotimia vizuri, una urefu wa mita 100, sasa vipangwe kwa mfuatano viwanja vinane halafu ongeza mita 29.8, ni kama mita 30 ndipo unapata urefu wa jengo la Burj Khalifa. Ni jengo refu kuliko yote duniani kwa sasa.
Burj Khalifa lilijengwa katika eneo la ekari tatu kama kivutio cha mji wa Dubai, lakini ikiwa na matumizi mbalimbali ikiwamo makazi ya watu 30,000, hoteli kubwa tisa, maduka makubwa yanayojulikana kwa jina la Dubai Mall, pamoja na eneo la ekari 12 lililojengwa bwawa linaloitwa ziwa la Burj Khalifa.
Burj Khalifa upande wa mbele jinsi linavyokuwa..
Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai, Omar Rajab Mjenga alisema katika mahojiano mafupi kuwa Dubai hawana mafuta wala mbuga za wanyama, kinachofanyika ni kuwekeza kwenye majengo yanayovutia.
Anasema kuwa kinachofanyika Dubai ni amri, kwamba Mfalme wa Dubai akisema kitu kifanyike, kinafanyika na hakuna mjadala, lengo likiwa tayari limeshapangwa.
Burj Khalifa jinsi linavyoonekana nyakati za usiku.
Mtawala alisema mbadala wa mafuta Dubai ni kuwa na kivutio cha utalii.
Balozi Mjenga anasema majengo marefu, mpangilio wa mji ni kivutio pekee cha utalii na sehemu kubwa ni fedha za wananchi zinazotoka mifukoni mwao.





Credit; Mwananchi



Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment