ZANZIBAR YAZIDI KUWABANA WATUHUMIWA WA ESCROW

Moja kati ya katuni kutoka kwa mkongwe Masoud Kipanya ikielezea kuhusiana na escrow.



Taasisi za kutetea haki za binadamu na kusimamia misingi ya Utawala Bora Zanzibar zimesema viongozi waliohusishwa na ufisadi wa Sh 306 bilioni kupitia Akaunti ya Tegeta Escrow
wakamatwe na kufikishwa mahakamani badala ya kufukuzwa kazi peke.
Msimamo huo umetolewa na Chama cha Wanasheria Zanzibar (ZLS) na Taasisi ya Utafiti na Sera za Kijamii Zanzibar (ZIRPP) baada ya waliotajwa katika sakata la escrow kung’oka na mmoja kusimamishwa kazi.
Rais wa ZLS, Awadhi Ali Said alisema viongozi waliohusika haitoshi kujiuzulu bila ya kufunguliwa mashtaka kwa vile kuna makosa ya jinai yamefanyika katika kashfa hiyo.
Alisema viongozi walioonyesha udhaifu wa kiutendaji na uzembe hadi kusababisha fedha hizo kuiibiwa wanapaswa kujiuzulu kulinda misingi ya uwajibikaji wa pamoja hata kama hawakuhusika moja kwa moja katika uchotaji wa fedha hizo.





Credit; Mwananchi
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment