FAHAMU KILICHOMTOA WASIRA CCM KWENDA NCCR MAGEUZI






STEPHEN WASIRA ambae ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu) pia ni Mbunge wa Bunda (CCM)  aongelea kuhusiana na mgogoro wake na Jaji Joseph Warioba uliotokana na kura za maoni ndani ya CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995, ndiyo uliomsukuma kujitoa chama tawala na kujiunga na NCCR-Mageuzi.

Hata hivyo,  amesema hajutii uamuzi wake huo kwa kuwa anaamini historia imeandikwa.
Wasira aliingia kwenye mgogoro na Jaji Warioba wakati mwanasheria huyo akiwa waziri mkuu na makamu wa kwanza wa rais katika Serikali ya awamu ya pili na Wasira akiwa Waziri wa Kilimo.
Wasira alisema hakwenda NCCR-Mageuzi kwa lengo la kufanya ushushushu na baadaye kurudi CCM kama alivyofanya mwaka 2000, bali alikwenda huko baada ya haki yake kuminywa na viongozi wa CCM wa wakati huo.
Alieleza kuwa baada ya uchakachuaji huo katika kura za maoni, aliamua kwenda Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam kukata rufaa, lakini hata huko hakutendewa haki, kwani rufaa yake iliwekwa kiporo na ingesikilizwa baada ya uchaguzi mkuu.
Mgogoro ulivyoanza
“Nataka mwelewe kwamba mimi sikwenda upinzani kwa sababu nilikuwa napingana na sera za CCM. Kwanza 1985 nilikuwa mbunge na ndiyo maana Rais Ali Hassan Mwinyi aliniteua kuwa waziri wa kilimo,” alisema Wasira na kuongeza;
“Mwaka 1990 niliacha kugombea kwa kumwachia Jaji Warioba. Kwa sababu kama utakumbuka mwaka 1985 Warioba alikuwa ameteuliwa kuwa mbunge na waziri mkuu na makamu wa kwanza wa rais.”
Wasira alisema aliamua kumwachia Jaji Warioba kwa kumheshimu kwani aliamini ingekuwa kampeni ngumu kwamba waziri mkuu anachuana na waziri wa kilimo, ingawa hata hivyo, alisema iwapo angeamua kuchuana naye angemshinda.
“Lakini lile jimbo lilikuwa la kwangu kwa sababu mimi ni kiongozi kutokea chini kwenda juu na mwenzangu Warioba ni mwanasiasa wa kutokea juu kwenda chini,” alisema.
Wasira ambaye alionekana kuukumbuka vizuri mgogoro huo alisema, “Hiyo ndiyo tofauti iliyopo. Kwa hiyo kama mimi ningeamua kuchuana naye, angeshindwa mwaka huo wa 1990. Sasa faida yenyewe iko wapi?” alihoji Wasira.
“Mimi nikaamua kujitoa si kwa kumwogopa Warioba, hapana. Hii ilinipa sifa nzuri kwa sababu Mwalimu (Julius Nyerere) aliniambia umefanya jambo la heshima sana
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment