JESHI LA POLISI NA WAANDISHI WA HABARI

moja ya picha katika matukio ya polisi na raia .




Kitendo cha Jeshi la Polisi kuzidi kuwapiga waandishi wa habari kimezidi kukithiri kila inapoitwa leo.

Tukio la kushambuliwa kwa waandishi watatu lilitokea juzi mbele ya ofisi za Wizara ya Mambo ya Ndani, kutaka kufahamu hatima ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliyekuwa anahojiwa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi kutokana na kauli aliyoitoa ya kuitisha maandamano nchi nzima yasiyo na kikomo kupinga kile kinachoendelea bungeni Dodoma.
Waandishi waliokutana na kadhia hiyo ni wa gazeti la Tanzania Daima, Josephat Isango, gazeti la Hoja, Shamimu Ausi na mpiga picha wa magazeti ya Serikali (TSN), Yusuf Badi ambao walijeruhiwa. Isango alijeruhiwa mguuni na Ausi usoni karibu na jicho.
Kitendo hicho kimetokea zikiwa zimepita siku mbili tangu kufanyika mkutano wa mashauriano kati ya vyombo vya dola na waandishi wa habari ambapo Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal alikuwa mgeni rasmi. Katika mkutano huo, si viongozi wa polisi au wawakilishi wake waliohudhuria huku Dk Bilal akitoa wito kwa vyombo hivyo kufanya kazi kwa kushirikiana bila kukwaruzana kwa lengo la kudumisha amani.
hata hivyo kitendo hicho kimelaaniwa vikali na taasisi mbalimbali, huku Chama cha Chadema na Maendeleo (CHADEMA) kikisisitiza kutositisha mpango wao wa kuandamana nchi nzima kupinga kuendelea kwa vikao vya Bunge Maalumu la Katiba.




Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment