wajumbe wa bunge la katiba wakiwa katika moja ya vikao vyao wakijadili kuhusiana na kupatikana kwa bunge la katiba mjini DODOMA. |
Hofu imetanda kuhusu uwezekano wa kuvunjika kwa Bunge Maalumu la Katiba, kutokana na hatua ya CCM kutumia wingi wao kutaka kupitisha utaratibu wa kupiga kura za wazi.
Baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo, wameshauri njia pekee ya kunusuru mchakato huo ni kwa CCM kukubali kukaa meza ya mazungumzo.
Wakati wajumbe hao wakitoa angalizo hilo, taarifa
zilizopatikana jana mjini Dodoma zilisema CCM, wameitisha kikao cha
dharura cha wajumbe wake wote leo saa 8:00 mchana kwa agenda ambayo bado
ni siri.
Habari hizo zinadai kuwa wajumbe ambao ni Wabunge
na Wawakilishi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, wametumiwa ujumbe
mfupi wa simu (SMS) wakitakiwa kuhudhuria kikao hicho bila kukosa.
“Mambo muhimu yatajadiliwa, Mwenyekiti wa Cocas
(umoja wa wabunge) anasisitiza mhudhurie bila kukosa, mahudhurio
yatazingatiwa,” unasomeka ujumbe huo ambao gazeti hili limeuona.
Baadhi ya wabunge wa CCM hususan wanaotoka Kanda
ya Ziwa wanaounga mkono kura ya siri, walidai kuwa kikao hicho huenda
kina nia ya kuwatisha ili walegeze msimamo wao.
“CCM wanaogopa kura za siri kwa sababu moja tu,
wakiiruhusu watakuwa hawana control (udhibiti) wa wajumbe kutoka
Zanzibar ambao wengi wanataka Serikali tatu,” alidokeza mbunge mmoja
ambaye hata hivyo, hakutaka jina lake litajwe.
Mbunge huyo alisema kwa tathmini yake, kama
utaratibu wa kura za siri utapita, karibu asilimia 80 ya wajumbe wote
kutoka Zanzibar, watapiga kura ya kupitisha rasimu ya muundo wa Serikali
tatu.
“Kwa hiyo CCM haitaki kabisa utaratibu wa kura za
siri, wanataka kura za wazi ama kura ya dhahiri ili waweze kuwa na
udhibiti wa wajumbe ili tusitoke nje ya msimamo wao,” alidai mbunge
huyo.
Hata hivyo, wakati CCM ikishikilia msimamo wa kura
za wazi katika kupitisha rasimu hiyo, wabunge wake wengi wa Tanzania
Bara na wale wa Zanzibar wanataka upigaji wa kura za siri.
Akizungumza na gazeti hili jana, James Mbatia
alitahadharisha kuwa msimamo wa CCM kulazimisha kura za wazi, siyo
kuwatendea haki Watanzania na huenda ikawa chanzo cha machafuko na
kukwama kupatikana Katiba Mpya.
“Kulazimisha matakwa ya CCM badala ya wananchi
itakuwa ni chanzo cha machafuko na Watanzania hatuko tayari kwa
machafuko wala kuona damu ya Mtanzania inamwagika,” maneno kutoka kwa James Mbatia.http://www.youtube.com/watch?v=EkEtBWIZ7Js
0 comments :
Post a Comment