MABINTI 12 WAKAMATWA WAKIWA NA DAWA ZA KULEVYA

Dawa za kulevya aina ya Cocaine.

Licha ya kampeni kubwa ya kupambana na kuzuia usafirishaji, uuzaji na matumizi ya dawa za kulevya nchini, bado Watanzania wameendelea kufanya biashara hiyo na katika kipindi cha siku 30 mabinti 12 wamekamatwa wakisafirisha dawa hizo ndani na nje ya nchi

Taarifa zilizothibitishwa na Kamishna wa Kikosi cha Kupamba na Dawa za Kulevya nchini, Godfrey Nzowa zinaonyesha kuwa idadi kubwa ya Watanzania waliokamatwa katika kipindi hicho ni mabinti wenye umri mdogo.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, mabinti wanane wamekamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Hong Kong na wanne katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam.
Kamishna Nzowa alisema ingawa vyombo vya habari na wafungwa walioko Hong Kong wamejaribu kuwashauri Watanzania wasifanye biashara hiyo, bado wamekuwa na ‘shingo ngumu.’
Alisema Januari 23, wanawake wawili, Rehema Ndunguru (31) na Moyo Ramadhani (31) walikamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere wakisafirisha dawa hizo kwenda Hong Kong.
“Rehema alikuwa amemeza pipi 78 ambazo ni sawa na kilo 1.2 na Moyo alitoa pipi 86 sawa na kilo 1.5,” alisema Kamanda Nzowa.
Alisema Februari 12, mwaka huu alikamatwa mwanamke mwingine Munira Mohamed (27) akiwa amemeza pipi zenye uzito sawa na kilo 1.
 
Februari 9, mwaka Halmati Tango (21) alikamatwa akiwa na pipi 76 zenye uzito sawa na kilo 1.3.
Nzowa alisema Halmat alikuwa akisafirisha dawa hizo kwenda Nigeria wakati Munira alikuwa akizipeleka Mombasa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment