Ripoti ya uchunguzi wa kashfa ya kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) ya uchotwaji wa Sh306 bilioni kwenye...
akaunti ya Tegeta Escrow, iliyoko Benki Kuu ya Tanzania (BoT) zimeibiwa na kuzua mambo.
Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi mkoani Dodoma limewatia mbaroni vijana wawili wanaotuhumiwa kusambaza mitaani ripoti ‘feki’ ya ukaguzi wa hesabu za fedha hizo uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusiana na kashfa hiyo.
Ripoti hiyo inadaiwa kuibwa na vijana hao katika Ofisi ya Katibu wa Bunge na kuichakachua kabla ya kuisambaza mitaani.
Vijana hao, ambao wanadaiwa kuwa ni baadhi ya watu waliomo katika kikosi cha waziri mmoja kilichoingia mjini Dodoma, wanadaiwa kusambaza ripoti hiyo ‘feki’ kwa kutumwa na waziri huyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alithibitisha polisi kuwashikilia vijana hao tangu juzi na kusema kuwa walipohojiwa, walikiri kupewa nyaraka hizo na mbunge, ambaye hata hivyo alikataa kumtaja kwa sababu za kiuchunguzi.
Pia Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alithibitisha kutoa taarifa polisi kuhusu vijana hao kumiliki nyaraka zenye mihuri ya ofisi yake isivyo halali.
Kamanda Misime alisema walikuwa wanawashikilia vijana hao, tulipata taarifa kutoka kwa Katibu wa Bunge kuwa kuna watu wanasambaza nyaraka kutoka Ofisi ya Katibu wa Bunge,” alisema Misime na kuongeza: “Baada ya taarifa hiyo, tulianza msako katika mji huu wa Dodoma na kufanikiwa kuwakamata vijana wawili.”
“Mmoja tulimkuta akiwa na nyaraka tatu, ambazo mbili zilikuwa na muhuri wa Ofisi ya Katibu wa Bunge.”
“Tulikwenda hadi katika hoteli aliyofikia na kufanya uchunguzi na tulipombana zaidi, alikiri kupewa na mbunge mmoja, ambaye kwa sasa jina lake tunalihifadhi kwa sababu ya uchunguzi.”
“Hatua tunayochukua sasa ni kuzipeleka karatasi hizi kwa mtaalamu wa maandishi kwa uchunguzi zaidi. Swali la kujiuliza kama zilikuwa za siri, je, huyu kijana alizipataje na kuanza kuzagaa mitaani?” alihoji Kamanda Misime.
Wakati vijana hao wakishikiliwa na polisi, hali bado ni tete ndani ya Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Hiyo ni kutokana na kuibuka madai kadhaa, ikiwamo kusukwa kwa mipango inayoelezwa kuwa ni ya hujuma ili kukwamisha uwasilishwaji wa ripoti sahihi ya uchunguzi wa kashfa hiyo.




Credit; Mwananchi
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment