ESCROW; MABALOZI WATAKA HATUA ZAIDI ZICHUKULIWE

Balozi wa Vatican nchini, Francisco Montecillo Padilla (kushoto) akizungumza na Balozi wa Saudi Arabia nchini, Hani Mominah wakati wa sherehe za mwaka mpya zilizoandaliwa kwa ajili ya mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao na mashirika ya kimataifa

Licha ya Rais Jakaya Kikwete kutoa ufafanuzi wa sakata la uchotaji fedha kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa Benki Kuu na kutangaza kuchukua hatua dhidi ya..
baadhi ya viongozi na watendaji, nchi wahisani wamesema bado suala hilo linawachanganya na wanasubiri tamko la Serikali.
Nchi hizo, ambazo zilizuia takriban Sh1 trilioni za ufadhili na kuchangia nakisi ya bajeti ya Serikali, juzi zilikiri kuanza kuruhusu sehemu ya fedha hizo baada ya baadhi ya maazimio ya Bunge la Jamhuri ya Muungano kuanza kutekelezwa, ikiwa ni pamoja na kumvua uwaziri Anna Tibaijuka, kumsimamisha kazi Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi na kumuweka kiporo waziri wake, Sospeter Muhongo na kusababisha Jaji Fredrick Werema kujivua wadhifa wake wa Mwanasheria Mkuu.
Tayari Rais Jakaya Kikwete ameshaeleza kuwa fedha hizo hazikuwa za Serikali.
Hata hivyo, Balozi wa Jumuiya ya Ulaya nchini, Timothy Clarke alisema kwamba Serikali imeonyesha jitihada za mwanzo, lakini wanasubiri kuona hatua kali zaidi zikichukuliwa pamoja na kuja na kauli moja kuhusu fedha hizo.
Alisema alichobaini ni kwamba wananchi wengi wanataka kujua hatima ya sakata hilo ndiyo maana walitumia vyombo vya habari kufanya mijadala mbalimbali kuzungumzia wizi wa fedha za escrow ambazo haijawekwa wazi kuwa ni za umma ama ni za Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL.
Balozi Clarke aliongeza kuwa kwa upande mwingine, Serikali imeonyesha tabia ya kusita katika kutoa uamuzi kwenye suala hilo na kwamba walitarajia kusikia tamko kali pamoja na tamko la kuzuia vitendo hivyo visiendelee.
Pia lieleza kuwa hadi sasa nchi nyingi hazijaipa fedha Tanzania kama zilivyokuwa zinatarajiwa kwa kuwa bado zinasubiri hatua zaidi kutoka serikalini.



Creidt; Mwananchi
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment