MWAKA MPYA NA UGUMU WAKE KWA WATANZANIA

 

Mwaka wa uchaguzi umeingia,watanzania wameupokea mwaka mpya 2015 huku tafakari kubwa ikiwa ni matukio makubwa yatakayotokea mwaka huu, mojawapo ni Uchaguzi Mkuu na kura ya maoni ya Katiba Inayopendekezwa.

Mbali na uchaguzi wa rais wa awamu ya tano, wananchi wataamua ama kuipitisha au kuikataa Katiba Inayopendekezwa, mambo ambayo wasomi, wanasiasa na wanaharakati wameonya kuwa yanatakiwa kuendeshwa na kusimamiwa kwa weledi na umakini mkubwa.
Vilevile, kutokana na matukio hayo kugharimu fedha nyingi, wataalamu wa uchumi wanatabiri kuwa mwaka huu utakuwa mgumu na itawalazimu Watanzania kufunga mikanda zaidi.
Pia, macho na masikio ya wananchi yako kwa vyama vya upinzani ambavyo vimeungana na kuzaa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuona kama vitasimamisha mgombea mmoja wa urais na katika nafasi za ubunge na udiwani kama vilivyokubaliana, ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992.
Maandalizi ya uchaguzi huo yanaanza mwezi huu kwa wapigakura kuandikishwa upya katika Daftari la Kudumu la Wapigakura, ambalo tangu mwaka 2009 halijawahi kuboreshwa na hivyo kusababisha wengi kushindwa kupiga kura katika uchaguzi wowote uliofanyika baada ya 2010.
Pengine jambo ambalo linasubiriwa kwa hamu na wananchi ukiacha Uchaguzi Mkuu na Katiba Mpya ambayo kampeni zake zitaanza Aprili 30, ni mchakato wa ndani ya vyama vya siasa wa kupata wagombea urais, hasa kutokana na mvutano ulioanza kujitokeza ndani ya CCM na mvutano unaotarajiwa ndani ya Ukawa.




Credit; Mwananchi
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment