WAGONJWA WA EBOLA WAKATAZWA KUTOKA NJE


ebola virus victims
Daktari akimpa matibabu muathirika wa ugonjwa wa Ebola katika moja vituo vya kutoa huduma kwa wagonjwa wa Ebola.

Serikali ya Sierra Leone imetangaza siku tatu za marufuku ya kutotoka nje kaskazini mwa taifa hilo, ili kuruhusu jitihada za kukabiliana na kuenea zaidi kwa ugonjwa hatari wa Ebola.

Msemaji wa serikali amesema kuwa maduka na masoko yatafungwa na hakuna magari ya abiria au pikipiki yatakubaliwa kwenye barabara za eneo hilo.
Sherehe za makanisa kuadhimisha sherehe za siku ya Krismasi pia zimepigwa marufuku katika ukanda huo.
Sierra Leone ni mojawapo ya mataifa ya Afrika magharibi ambayo yalikumbwa kwa sehemu kubwa na ugonjwa huo wa ebola ambao pia umeleta maafa makubwa mpaka sasa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment