MUIGIZAJI AZABWA KOFI KWA KUVAA NGUO FUPI

Mwigizaji maarufu wa Bollywood ambaye pia ni mwanamitindo, Gauhar Khan, alizabwa kofi wakati wa shughuli ya kurekodi makala ya kipindi kuhusu maisha yake.

Mwigizaji huyo alizabwa kofi na mmoja wa waliokuwa wanatazama kipindi hicho eti kwa kuwa alikuwa amevalia nguo fupi sana.
Polisi walimkamata mwanamume mwenye umri a miaka 24 kwa kumshambulia mwigizaji huyo wakati wa kurekodi kipindi kijulikanacho kama , ''India's Raw Star'' mjini Mumbai.
Mwanamume aliyemshambua muigizaji huyo alinukuliwa akimkaripia na kumwambia, kwamba kwa kuwa yeye ni mwanamke wa kiisilamu hapaswi kuvalia nguo fupi kama ile.
Mwanamume huyo alitarajiwa kufikishwa mahakamani Jumatatu.
Tukio hilo lilitokea Jumapili, wakati wa kurekodiwa kwa makala ya mwisho ya kipindi hicho.
Uchunguzi umeonyesha kuwa mtu mmoja kutoka kwa mashabiki, alianza kumkejeli Khan ambaye naye hakumsaza kwani alianza kujibizana naye. Katika majibizano yao, mwanamume huyo alimzaba kofi Khan.
Duru zinasema kuwa walinzi waliokuwa katika eneo hilo walimshinda nguvu mwanamume huyo ambayo walimkabidhi kwa polisi.
Polisi walimshitaki mwanamume huyo kwa kitendo cha kumzaba kofi Khan ambaye ameigiza katika filamu nyingi tu ikiwemo, 'Rocket Singh: Salesman of the Year.'




Credit; BBC
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment