KOCHA WA DORTMUND ASEMA HAONDOKI

Klopp alisema hana mipango yoyote ya kung'atuka kutokana na matokeo hayo mabaya


Ni mara ya kwanza tangu msimu wa 2007 na 2008, ambapo Dortmund wameshikilia mkia lakini Klopp ambaye pia aliiongoza klabu hiyo katika fainali ya Champions League miezi 18 pekee iliyopita, amesema wako tayari kujinyanyua upya na kusonga mbele.
Alipoulizwa kama alikuwa na fikra zozote za kuondoka, Klopp aliiambia televisheni ya Sky kuwa na namnukuu “kama ni suala la bahati pekee na iwe ni kocha mpya atatimiza hilo, basi niileze hivyo na kisha nitaondoka. Lakini kama hakuna yeyote atakayejitokeza na kuniambia kuwa kuna mtu atakayeweza kuimarisha matokeo, basi siwezi kuondoka”. Mwisho wa nukuu.
Klopp anasema hajamzuia yeyote lakini hawezi kung'atuka kama hakuna suluhisho bora. Na kwa sasa hilo ni jukumu lake na analikubali. Dortmund, ambao tayari wamefuzu katika duru ya mchujo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, sasa wamepoteza mechi nane kati ya 13 msimu huu. Huku wakiwa na safu dhaifu ya ulinzi, ukosefu wa mabao na msururu wa majeruhi, wakiwemo Marco Reus na mabeki Mats Hummels na Sokratis Papastathopolous, BVB wameshinda mechi moja tu kati ya kumi za Bundesliga na wana points 11 pekee.




Credit; DW
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment