MAAFA YA MVUA;WATU ZAIDI YA 300 WAHOFIWA KULA SUMU



Zaidi ya watu 323 wakazi wa Kijiji cha namba 9 katika Kata ya Bulyanhulu wilayani Kahama mkoani Shinyanga, wanahofiwa kula sumu kali aina ya sodium cyanide inayotumiwa katika Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu unaomilikiwa na Kampuni ya Acacia.

Hali hiyo imetokana na mvua kubwa kunyesha na kubomoa bwawa kubwa la ndani ya mgodi huo wa Bulyanhulu, ambalo hutunza sumu hiyo na kusababisha maji hayo kutiririkia kwenye bwawa la nje linalotumiwa na wananchi.
Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Acacia, Necta Foya alisema jana kuwa, maji hayo yalibomoa pia bwawa la nje na kwenda vijijini.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya alisema baada ya maji hayo yanayosadikiwa kuwa na sumu kubomoa bwawa la nje yalisambaa pia kwenye mashamba ya watu.
Mpesya, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kahama, alisema katika eneo hilo takriban hekta 15 za mpunga zimeathiriwa na sumu hiyo, zikiwamo bustani za nyanya.
Mpesya alisema ili kunusuru maisha ya wananchi hao, huduma zote za maji ya kunywa mifugo na binadamu kwenye visima na mabwawa zimefungwa na tayari mgodi huo umevuta kwa muda maji ya bomba ambayo sasa wananchi hao wanayatumia.
Hata hivyo, Mpesya alisema tayari watalaamu wa afya na mazingira wamechukua sampuli ya maji hayo pamoja na nyanya kwenye bustani inayodhaniwa kunyonya maji yenye sumu hiyo na kupeleka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali
Pamoja na hali hiyo, jana wananchi wote wanaoishi eneo hilo walipelekwa Hospitali ya Wilaya ya Kahama kupimwa afya zao, zoezi ambalo lilikuwa likiendelea kufanywa na madaktari wote kutoka halmashauri tatu za Wilaya ya Kahama.
Alisema uamuzi huo wa kuwapima wananchi unatokana kuhisi kuwa wametumia maji yaliyochanganyika na sumu hiyo.
Pia, Mpesya alisema kamati yake ilikubaliana na watu hao wapimwe wakati hatua nyingine zikiendelea kufanywa ikiwa ni pamoja na kusubiri majibu kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili kujua sumu hiyo imeingia kwenye eneo hilo kwa kiasi gani.



Credit; Mwananchi
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment