Serikali ya nchini Afrika Kusini inasema
kuwa watu miamoja na kumi na tano(115) wengi wao wakiwa raia wa Afrika
Kusini, walifariki dunia baada ya kanisa kuporomoka nchini Nigeria.
Idadi kamili ya raia wa Afrika Kusini waliofariki ilikuwa 84.Ndege iliyowabeba manusura wa mkasa huo, kumi na sita (16) kati yao wakiwa wamejeruhiwa vibaya, imewasili mjini Pretoria.
Lakini pia zaidi ya watu 300 kutoka Afrika Kusini walikuwa wametembelea kanisa hilo la "All Nations" mjini Lagos, ambalo linaongozwa na mhubiri T.B. Joshua.
Inaarifiwa kuwa jengo hilo liliporomoka kutokana na ujenzi mbovu.
Mhubiri TB Joshua, amezua wasiwasi baada ya kuzungumzia juu ya kuona ndege iliyokuwa inazunguka juu ya kanisa hilo kabla ya jengo lenyewe kuporomoka.
0 comments :
Post a Comment