TETESI ZA MAWINDO YA USAJILI BARANI ULAYA

Manchester United inaweza kutumia mpaka kiasi cha pauni milioni 350 kwa kipindi cha miaka miwili katika kusajili wachezaji wapya.

Hii inaweza kufikiwa kama watafanikiwa kuwasajili kiungo Kevin Strootman 24,toka roma, na beki wa Borussia Dortmund Mart Hummels, 25,pia inasadikika kocha Louis van Gaal anamtaka beki wa kulia wa Southampton Nathaniel Clyne, 23.
Arsenal wako tayari kurekebisha safu yao ya kiungo kwa kumuwania kiungo Morgan Schneiderlin, toka Southampton kwa dau la pauni milioni 15 pia wako tayari kutoa pauni milioni 8 kwa beki Tyrone Mings, 21,wa Ipswich Town.
Inter Milan wanaangalia uwezekano wa kumsajili mshambulaiji Joel Campbell, wa Arsenal raia wa Costa Rica pamoja na kiungo wa Tottenham Erik Lamela 22.
Henrique Pompeu wakala wa mshambuliaji wa Colombia Jackson Martinez 28, ameeleza kuwa mteja wake huyo hatoondoka katika timu yake ya Fc Porto japo timu za Arsenal, Liverpool and Tottenham zimekua zikimuwania.
Meneja wa Newcastle Alan Pardew, anawasiwasi nyota wake Moussa Sissoko,ataondoka St James' Park kuelekea Arsenal katika usajili wa dirisha dogo mwezi januari.
Real Madrid na Paris St-Germain wanapigana vikumbo kuweza kupata saini ya mshambuliaji Eden Hazard.Huku chelsea wakiwa tayari kumboreshea kandarasi yake ya sasa nyota huyo wa ubelgiji mwenye miaka 23.
Kiungo wa kibrazil Luca Silva,21,anayechezea klabu ya Cruzeiro yuko tayari kuzikata ofa za Manchester United na Arsenal ili kujiunga na miamba wa hispania Real Madrid.
Timu Leicester City itajaribu kutaka kumrejesha tena kwenye ligi ya Epl mshambuliaji Jermain Defoe, 32,toka klabu ya Toronto Fc.




Credit; BBC
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment