MABIBIHARUSI ZAIDI YA 100 WATOWEKA

Polisi nchini China wanafanya uchunguzi wa kuwasaka mabibi harusi zaidi ya mia moja wenye asili ya Vietnam ambao walipotea katika kijiji kimoja masikini kaskazini mwa jimbo la Hebei baada ya kuolewa .

Makuwadi waliowauza mabibi harusi kwa wanaume wameshangazwa na kitendo cha kupotea kwa mabibi harusi pamoja na pesa walizozipata makuwadi pia kupotea.
Wanawake hao walikuwadiwa kwa gharama ya dola 16,000 kila mmoja.
Lakini wadadisi wa mambo wanadai kwamba wanaume wa kichina walioko mijini wanapaswa kuwa na fedha za kutosha ili kuwavutia wanawake wa Kichina,na hivyo imewalazimu wanaume wa kichina kununua wanawake kutoka nje ya nchi hiyo kama Vietnam,Cambodia na Burma , zoezi linaloonekana kushika kasi kila uchao wakilenga vijiji hohehahe.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment