Ripoti kutoka kaskazini-mashariki mwa Nigeria zinaarifu kuwa kundi la wapiganaji Waislamu la Boko Haram, limefanya mashambulio mawili makubwa katika siku chache za karibuni ambapo watu karibu 100 wameuwawa.

Kiongozi mmoja katika jimbo la Borno alisema kuwa wapiganaji waliuwa wauza samaki karibu 50 karibu na kijiji cha Doron Baga, kando ya Ziwa Chad.
Alisema wapiganaji wa Boko Haram wameweka kizuizi kwenye njia ya kuelekea Chad na kuwakamata wachuuzi waliokuwa wakienda kununua samaki.
Katika tukio jengine hapo awali watu karibu 50 waliripotiwa kuwa waliuwawa karibu na mpaka wa Cameroon pale Boko Haram walipovamia kijiji cha Azara Kuya, siku ambapo soko huwa na watu wengi.




Credit; BBC
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment